Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Arsenal imesahau namna ya kushinda'' – Cech

Jumatatu , 24th Sep , 2018

Mlinda mlango wa Arsenal, Petr Cech amesema klabu hiyo imepoteza hali ya ushindi kutokana na kutoshinda mataji kwa kipindi kirefu.

Mlinda mlango, Petr Cech

Arsenal ilishinda taji lake la mwisho la ligi kuu nchini Uingereza, EPL msimu wa 2003/04 na haijafanikiwa kufuzu michuano ya Klabu bingwa Ulaya kwa misimu miwili ya mwisho, jambo ambalo Cech anaamini linaifanya klabu hiyo isahau namna ya kushinda mataji.

Cech ana mataji manne ya EPL, ambapo yote ameshinda akiwa na klabu ya Chelsea kabla ya kujiunga na Arsenal mwaka 2015.

“ Kwa klabu yoyote ambayo inashinda vikombe katika miaka ya karibuni inakuwa na kikosi ambacho kinajua namna ya kushinda mechi zao na mataji, hilo unaweza ukaliona wazi uwanjani ”, amesema Cech.

“ Inachukua muda kama Tiger Wood ambaye amechukua miaka mitano bila kushinda taji lolote kubwa, na kadri miaka inavyoongezeka na ugumu unavyozidi kuongezeka pia. Klabu hii haijashinda ubingwa kwa miaka 10 sasa, kwahiyo inabidi turudi nyuma tufahamu namna gani ya kushinda ”, ameongeza Cech.

Mchezo uliopita wa EPL ulikuwa bora sana kwa Petr Cech ambaye mara kadhaa amekuwa akilaumiwa kwa udhaifu katika miguu yake, aliisaidia Arsenal kushinda mchezo wake wa tano mfululizo katika mashindano yote baada ya kupoteza mechi mbili za awali za ligi.

 Golikipa huyo anaamini kuwa Arsenal itashinda mataji baada ya muda mfupi kutokana na maendeleo anayoyaona kupitia kwa kocha wake mpya, Unai Emery ambaye wameanza naye tangu msimu ulipoanza.

“ Tunafanya kazi, tunajaribu kufanya kila namna na kukusanya alama kadri inavyowezekana huku tukiendelea kuwa bora katika kila mchezo. Tuna furaha na alama tunazozipata  ”.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto