Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya Simba, Mtibwa wawajua wamiliki wa kombe

Jumatatu , 3rd Dec , 2018

Klabu ya soka ya Mtibwa Sugar ambao ni wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika, wana kibarua cha kusaka taji hilo mbele ya mabingwa wapya Raja Casablanca ambao wametwaa ubingwa huo jana usiku.

Kikosi cha Mtibwa Sugar, chini kulia ni wachezaji wa Raja Casablanca wakishangilia ubingwa.

Raja Casablanca wameibuka mabingwa wa kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2018 licha ya kufungwa mabao 3-1 na AS Vita Club ya DR Congo kwenye mchezo wa fainali ya pili uliopigwa usiku wa kuamkia leo.

Raja imebebwa na ushindi wa mabao 3-0 ilioupata kwenye fainali ya kwanza hivyo kuwa na ushindi wa jumla ya mabao 4-3 na kutawazwa kuwa mabingwa ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu walipofanya hivyo miaka 15 iliyopita.

Kwa upande wa kocha wa Casablanca, Juan Carlos Garrido yeye amekuwa kocha wa kwanza kuchukua kombe la shirikisho akiwa na vilabu viwili tofauti baada ya kufanya hivyo akiwa na Al Ahly ya Misri mwaka 2014.

Mtibwa ambao wapo kwenye michuano hiyo walishinda 4-0, mchezo wao wa kwanza raundi ya awali dhidi ya Northern Dynamo ya Ushelisheli na tayari wameshasafiri kwenda kwenye mchezo wa marejeano utakaopigwa Jumatano Disemba 5.

Kwa upande wa klabu bingwa tayari Simba wameshajua klabu inayoshikilia taji hilo ambayo ni Esperance ya Tunisia. Simba nao wapo nchini eSwatini kurudiana na Mbabane Swallows ambao waliwafunga mabao 4-1.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa