Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Barcelona yafuzu fainali mbele ya wagombe urais

Alhamisi , 4th Mar , 2021

Klabu ya soka ya FC Barcelona imetinga fainali ya michuano ya kombe la mfalme (Copa del rey), baada ya kuifunga Sevilla mabao 3-0 kwenye mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa magoli 3-2.

FC Barcelona

Ushindi wa magoli 3-0 uliwafanya Barcelona kupindua matokeo baada ya kupoteza mchezo wa mkondo kwa bao 2-0. Mchezo huo ulichezwa kwa dakika 120 baada ya dakika 90 kumalizika kwa Barcelona kuongoza 2-0 na kufanya matokeo ya jumla kuwa 2-2 na hivyo dakika 30 zikaongezwa ili kumpata mshindi wa jumla.

Mabao ya ushindi ya Barcelona katika mchezo huo ambao ulipigwa katika dimba la Camp Nou yalifungwa na Ousmane Dembele dakika ya 12, Gerard Pique dakika ya 90 na Martin Braithwaite dakika ya 95. Mchezo huu pia ulishuhudiwa na wagombea wa Urais wa klabu hiyo wote watatu Joan Laporta, Toni Freixa na Victor Font.

Barcelona wamefuzu kucheza fainali ya mashindano haya kwa mara ya 42 na wakiwa wanauwinda ubingwa wa 31 na mpaka sasa ndio wanashikiria rekodi ya kutwaa ubingwa wa michuano hii mara nyingi zaidi, wakiwa wametwaa ubingwa wa michuano hii mara 30.

Barcelona sasa watakutana na mshindi wa jumla wa mchezo wa nusu fainali ya pili kati ya Levante na Athletic Bilbao.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu