Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bocco aitaja ndoto yake kubwa katika soka

Alhamisi , 6th Dec , 2018

Mshambuliaji na nahodha wa klabu ya Simba, John Bocco amefunguka juu ya ndoto yake kubwa ya kucheza soka kimataifa muda wowote endapo ataipata nafasi hiyo.

John Bocco

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29, yupo nchini eSwatini na klabu yake ya Simba wakipata mapumziko mafupi baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Mbabane Swallows ya nchini humo wikiendi iliyopita.

Akizungumzia kuhusu ndoto yake ya kucheza soka la kimataifa, John Bocco amesema, "bado naona nina nafasi ya kucheza soka nje ya Simba na Tanzania, ninaamini nikipata nafasi nitaitumikia vizuri".

Ikumbukwe kuwa Bocco hajawahi kucheza soka nje ya nchi, ambapo mpaka sasa amevitumikia vilabu viwili pekee vya ligi kuu Tanzania bara, ambavyo ni Azam FC na Simba SC.

Katika vilabu hivyo viwili, Bocco amefanikiwa kuweka historia ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa ligi kuu Tanzania bara TPL, akiwa amefunga zaidi ya mabao 100 tangu mwaka 2008 alipoanza kucheza ligi kuu akiwa na Azam FC.

Bocco ambaye yupo na kikosi cha Simba eSwatini baada ya kumaliza kazi dhidi ya Mbabane Swallows, ameeleza kuwa endapo akipata nafasi hiyo hataweza kuipoteza kirahisi.

Wakati huo kikosi cha Simba kinatarajia kuwasili leo nchini baada ya kufanikiwa kutinga hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika kwa ushindi wa jumla ya mabao 8-1 dhidi ya Mbabane Swallows.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine