Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bocco asimulia alivyotendwa mitandaoni

Jumatatu , 22nd Mei , 2017

Nahodha wa Azam FC, John Bocco, hivi karibuni amejikuta akiingia matatizoni na uongozi wa klabu yake baada ya wajanja wa mtandaoni kumzidi ujanja.

Nahodha wa Azam, John Bocco

Taarifa kutoka klabuni hapo zimedai kuwa ukurasa wa Instagram wa Bocco, Ijumaa iliyopita ulivamiwa na matapeli wa mtandaoni na kuanza kuandika mambo mbalimbali kuhusiana na mchezaji huyo, jambo ambalo liliushitua uongozi wa klabu hiyo.

Moja kati ya mambo hayo yaliyoandikwa katika ukurasa huo ni: “Kuna wakati wa kuondoka hata kama hujui pa kwenda, ondoka wajue thamani yako.”

Maneno hayo yaliwachanganya vilivyo viongozi wa timu hiyo, baada ya kuyaona katika ukurasa huo, jambo ambalo lilisababisha wamuulize alikuwa akimaanisha nini.

Bocco amesema kuwa, hali hiyo ilimsababishia usumbufu mkubwa kwani watu wengi waliamini kuwa yeye ndiye aliyeandika maneno hayo licha ya kuwaambia ukweli kuhusiana na kilichotokea.

“Nawaomba watu wote waelewe kuwa sina tatizo na Azam na wala siyo mimi niliyeandika maneno hayo, bali ni matapeli ambao wamevamia ukurasa wangu wa Instagram tangu juzi (Ijumaa) na wamekuwa wakiandika mambo yao hayo huku nikiona.

“Hata hivyo nimeshatoa taarifa sehemu zinazohusika lakini pia nimeamua kufungua ukurasa mwingine wa Instagram,” alisema Bocco ambaye anadaiwa mkataba wake na Azam umemalizika, hivyo inadaiwa kuwa ametumia mbinu hiyo ili kushtua uongozi wake uweze kumpatia mkataba mwingine.

Alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema: “Huo ni uzushi tu ambao hauna ukweli wowote, mimi bado nina mkataba na Azam na kama utamalizika na wakiwa bado wananihitaji wataniambia, hivyo siwezi kufanya hivyo hata siku moja.”

Viongozi wa Azam FC hawakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hilo, kutokana na simu zao za mkononi kuita tu bila ya kupokelewa.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava