Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chelsea, heri punda afe mzigo ufike

Ijumaa , 13th Jan , 2023

Todd Boehly anakaribishwa kwenye ulimwengu wa 'stress', licha ya pesa zake zote lakini moja ya kitu kinamnyima usingizi hivi sasa ni Chelsea, usajili bora anaendelea kuufanya lakini matokeo bado magumu, hiki kitu huwa kinawapa shida sana matajiri hasa kwenye biashara zao.

Kocha wa Chelsea, Grahm Potter na nahodha Cesar Azpilicueta

Mashabiki wengi wa Chelsea wanaamini angekuwepo bosi Roman Abramovich asingekubali kudhalilishwa namna hii. Wanakumbuka urejeo wa pili wa Jose Mourinho pale darajani, alishinda ubingwa wa ligi lakini baada ya mechi 18 za msimu uliofuata, Roman Abramovich akamla kichwa kabla ya sikukuu ya Christmas 2015 kwasababu yeye alikuwa mtu wa matokeo na ndiyo maana Chelsea imekuwa kubwa na kufikia hapa ilipo kuwa na mataji 2 ya Klabu Bingwa Ulaya kuizidi Arsenal na taji moja nyuma ya Man United.

Kama hiyo haitoshi msimu 2016/17 Chelsea ilishinda ubingwa wa EPL na FA Cup chini ya Antonio Conte, halafu niulize nini kilitokea msimu uliofuatia!!. Conte alitimuliwa kwa kuikosesha Chelsea nafasi ya kushiriki Klabu Bingwa Ulaya.

Kwenye miaka takribani 19 ya Abramovich pale Chelsea ameajiri makocha 13, lakini ndiyo timu yenye mafanikio makubwa ya ndani na nje, kutokana na mtazamo tu wa Abramovich. Bwana Todd Boehly  ameamua kuja na mfumo tofauti wa kuamini mipango ya muda mrefu, ndiyo maana hata bodi yake imekuja na kauli ya kumlinda kocha Graham Potter licha ya matokeo mabaya anayopitia.

Lakini tunamkumbusha kuwa hakuna kocha Muingereza aliyechukua ubingwa wa EPL tangu Sir Alex Ferguson alipofanya hivyo mwaka 2013. Ni yeye tu bwana Boehly kuamua 'Punda afe mzigo ufike' ili mashabiki waendelee kula burger au kuwa baridi kusubiri project ambayo itazaa matunda baada ya miaka kadhaa huku akiwalisha kisamvu cha kwetu Nakapanya !!

Imeandikwa na @manafi_daimu   
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto