Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

EBOLA yavuruga michuano ya kimataifa ya Rollball

Jumamosi , 22nd Nov , 2014

Kufuatia bara la Afrika kukumbwa na janga la ugonjwa wa Ebola ambao umesababisha vifo kwa maelfu ya watu barani humu hasa kwa nchi zilizokumbwa na ugonjwa huo shirikisho la kimataifa la mchezo wa Rollball duniani limesogeza mbele mashindano

Michuano ya mchezo wa rollball kwa nchini za Afrika na Asia AFRO-ASIAN Championships iliyokuwa ifanyike jijini kampala mwishoni mwa mwezi huu imeahirishwa mpaka mwakani mwezi wa nne baada ya timu za kutoka bara la Asia kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao kwa sasa umeshika kasi kubwa katika baadhi ya mataifa barani Afrika

Mashindano hayo yalipangwa kupigwa jijini Kampala Uganda kuanzia Novemba 28 mwaka huu na hivyo sasa yatafanyika mwezi wa Nne katika mji huo huo wa Kampala lakini safari hii zikishiriki nchi za Afrika pekee

Mjumbe wa chama cha rollball Tanzania ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya rollball ya Tanzania Feruzi Juma ameiambia muhtasari wa michezo kuwa pamoja na hali hiyo wao bado wanaendelea kujiandaa na mashindano yoyote yatakayojitokeza mbele yao na bahati pekee katika kipindi hiki ambacho mashindano hayo yamesogezwa mbele timu yao imepata mwaliko wa kucheza mchezo mmoja na wenzao wa Kenya mchezo ambao utafanyika kati ya mji wa Arusha au Nairobi mapema mwezi ujao

Feruzi ametumia fulsa hiyo kuwashukuru wadhamini na wadau mbalimbali waliojitokeza kutoa misaada yao hasa suala la nauli na vifaa ambavyo watavitumia katika mashindano mbalimbali lakini pia bado wanakaribisha misaada zaidi katika nyanja mbalimbali ili wajiandae vema na hatimaye wakafanye vizuri katika michuano hiyo.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu