Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Eto'o kuhitimishia safari yake nchini Ufaransa

Jumatatu , 13th Aug , 2018

Nyota wa zamani wa Cameroon Samuel Eto'o mwenye miaka 37, amethibitisha kuwa yupo kwenye mazungumzo na klabu kadhaa za Ufaransa akiwa na mpango wa kucheza ligi hiyo kwa miaka miwili ijayo kabla ya kustaafu rasmi.

Samuel Eto'o

Eto'o ambaye anashikilia rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Cameroon akifunga mabao 56 kwenye mechi 118 alizocheza kwenye timu ya taifa, endapo atapata timu basi itakuwa ni ya 13 katika maisha yake ya soka ambapo safari yake ilianza zaidi miaka 20 iliyopita katika klabu ya Real Madrid mwaka 1997.

Hata hivyo Eto'o hakufanikiwa sana na Real Madrid kabla ya dunia kumtambua zaidi katika miaka 2004 na 2009 akiichezea Barcelona ambako alifunga mabao 130 katika michezo 199 huku akishinda La Liga mara 2 na UEFA mara 2. Mbali na Barcelona Eto'o alipata mafanikio ya kutwaa Serie A na UEFA akiwa na Inter Milan msimu wa 2009/10 chini ya kocha Jose Mourinho.

Mbali na kucheza ligi za La Liga na Serie A, Eto'o ni moja ya wachezaji wachache ambao wamebahatika kucheza ligi kubwa tatu duniani, akicheza pia kwenye ligi kuu ya England katika klabu za Chelsea na Everton na kumfanya awe amechezea klabu 12 zikiwemo mbili za Uturuki Antalyaspor na Konyaspor.

Mwaka 2011 Eto'o aliweka rekodi ya kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani alipotoka Inter Milan na kujiunga na Anzhi Makhachkala ya Urusi. Hata hivyo mara baada ya nyota huyo kuweka wazi mpango wake huo klabu kadhaa ikiwemo PSG zimeripotiwa kuwa huenda ndio yupo nayo kwenye mazungumzo.

Eto'o ni miongoni mwa wachezaji wachache wenye miaka 37 ambao bado wanataka kucheza soka la ushindani na huenda mpango wake ukatimia kwani dirisha la usajili nchini Ufaransa linafungwa Agosti 31 saa 6:00 usiku. Licha ya kutokuwa na timu kwasasa lakini Eto'o anatajwa kuwa na thamani ya Euro milioni 1 zaidi ya shilingi bilioni 26.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava