Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Gwiji wa zamani wa Yanga afariki dunia 

Jumatatu , 25th Mei , 2020

Aliyewahi kuwa mchezaji na Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga, Lawrence Mwalusako amefariki dunia leo Asubuhi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.

Yanga

Taarifa hiyo imethibitishwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wachezaji Tanzania, Mussa Kisoki ambapo amesema kuwa Mwalusako alikuwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji.

Katika maisha yake ya soka, Lawrence Mwalusako aliazia katika klabu ya Waziri Mkuu ya Dodoma kisha akajiunga na Yanga ambapo baada ya kustaafu alikuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo.

Mussa Kisoki amemzungumzia Mwalusako kuwa ni mtu mcheshi tangu alipokuwa mchezaji na hata katika uongozi wake, pia alisifika kwa kusimamia kwa umakini mipango mbalimbali, akitaja mfano kuwa alikuwa hana masihara hata katika masuala ya mazoezi ya klabu.

Taratibu za kuchukua mwili zinaendelea na msiba huo utakuwepo Ubungo Jijini Dar es Salaam, ambapo kwa mujibu wa Kisoki, familia itatoa taarifa rasmi baada ya taratibu zote kukamilika.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu