Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hukumu ya Mkude yaghairishwa mpaka akapimwe Afya

Jumanne , 8th Jun , 2021

Kamati ya nidhamu ya klabu ya Simba imeghairisha tena hukumu ya mchezaji wake Jonas Mkude iliyopangwa  kusomwa Juni 7, 2021 juu ya tuhuma za utovu wa nidhamu anazoshutumiwa kiungo huyo mkongwe kikosini.

Kiungo wa wekundu wa msimbazi Simba, Jonas Mkude anayetuhumiwa kwa kuwa na utovu wa nidhamu klabuni kwa mara ya pili.

Taarifa ya kughairisha kusomwa kwa hukumu hiyo ilitolewa usiku wa kuamkia leo na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kamanda Mstaafu, Suleiman Kova kupitia taarifa ya wazi kwa umma ambayo iliwekwa kwenye ukurasa wa mitandao ya kijamii ya klabu hiyo.

Taarifa kamili ya kughairishwa kwa hukumu hiyo inasomeka kama ifuatavyo;

(Taarifa kwa umma iliyotolewa na kamati ya nidhamu ya klabu ya Simba chini ya Mwenyekiti wake kamanda Mstaafu, Suleiman Kova).

Suala la kamati hiyo kughairisha hukumu kwa kile kilichoelezwa ni kuiagiza menejimenti ya Simba kuelekezwa kumpima Afya mchezaji huyo na ripoti ikitoka ndiyo itawezesha hukumu kamili kutoka imepokelewa kwa namna tofauti na wafuatiliaji wa soka nchini wengine wakihusisha utata wa utimamu wa akili wa mchezaji huyo jambo ambalo limewacha njia panda.

Hii ni mara ya pili Mkude kufikishwa kwenye kamati ya nidhamu, kwani mwezi wa pili mwaka huu alishutumiwa na makosa mawili ya kutohudhuria semina ya wachezaji n akuchelewa kufika kambini mambo yaliyopelekea kulimwa faini ya milioni mbili ikiwa baada ya kusimamishwa kwa muda wa mwezi mmoja na kupewa onyo kali la kutorudia makosa ndani ya miezi sita.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine