Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jota ni mchezaji wa kiwango cha Dunia- Klopp

Ijumaa , 21st Jan , 2022

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amemsifu mshambuliaji wake Diogo Jota kwa kiwango bora baada ya kufunga mabao 2 kwenye ushindi wa 2-0 walioupata kwenye mchezo wa nusu fainali ya kombe la Ligi Carabao CUP dhidi ya Arsenal. Na sasa watacheza fainali dhidi ya Chelsea.

Diogo Jota kushoto akipongezwa na kocha Jurgen Kloop

Ushindi huo wa mabao 2-0 ulitosha kuifanya Liverpool kukata tiketi ya kucheza fainali ya Carabao Cup na ulikuwa ni mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali ya michuano hiyo mabao yote mawili ya Liverpool yamefungwa na Diogo Jota dakika ya 19 na 77. Na sasa Liverpool wataminyana na Chelsea katika mchezo wa fainali Februari 27, 2022.

Mara baada ya mchezo huo kocha wa Liverpool Mjerumani Jurgen klopp akasifu kiwango bora cha Jota na umuhimu wa magoli aliyofunga jana hususani kipindi hiki ambacho Mo Salah na Sadio Mane hawapo kwenye kikosi.

"Wow, yupo kwenye kiwango bora,Tuliamini alipofika kwenye klabu atatusaidia kwa kiasi kikubwa. Mawazo yake na ubora wake ndivyo vilivyotufanya kumsajili.Tangu alivyojiunga nasi amepiga hatua, amekuwa mshambuliaji wa kiwango cha Dunia. Amesema Klopp.

Jota kafikisha mabao 14 kwenye michuano katika michezo 27 msimu huu, Lakini pia amefunga jumla ya mabao 27 katika michezo 57 tangu alipojiunga na klabu hiyo msimu uliopita wa 2020-21. Liverpool imekata tiketi ya kucheza fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-0 kwenye michezo ya mikondo miwili ya nusu fainali mchezo wa mkondo wa kwanza ulimalizika kwa suluhu 0-0 katika Dimba la Anfield.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava