Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lipuli yawaacha nyota wake

Jumatano , 16th Mei , 2018

Timu ya Lipuli FC inatarajiwa kushuka katika dimba la Manungu Turiani Mkoani Morogoro kuvaana na Mtibwa Sugar huku ikiwa inawakosa nyota wake sita kutokana na sababu mbalimbali zilizokuwa nje ya uwezo wao.

Hayo yamebainishwa na Kocha wa Lipuli, Seleman Matola wakati akizungumzia maandalizi ya mwisho ya kikosi chake kinachoenda kutafuta alama tatu mbele ya Mtibwa Sugar kwenye muendelezo wa kumaliza michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa mwaka 2017/18 na kuwataja nyota hao kuwa ni Jamali Mnyate, Stephen Mganga, Golikipa Yusuf, Fred Tangaru, Omega pamoja na Emmanuel Kichiba. 

"Tunaendelea vizuri maandalizi yetu dhidi ya Mtibwa Sugar japo nina amini mechi hii itakuwa ngumu sana kwa sababu Mtibwa ni miongoni mwa timu ngumu katika ligi kuu. Katika mchezo wa leo tutawakosa baadhi ya wachezaji kutokana na kuwa majeruhi wengine wana kadi za njano pamoja na kuwepo na matatizo ya kifamilia", amesema Matola.

Aidha, Matola amesema japokuwa timu yake itawakosa wachezaji hao lakini imejipanga vizuri kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika mchezo huo ili iweze kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi.

Lipuli FC kwa sasa inashikilia nafasi ya 8 kibindoni ikiwa na alama 32 kwa michezo 27 huku Mtibwa Sugar yenyewe ikishika nafasi ya 6 kwa alama 37 yenyewe ikiwa imecheza michezo 27.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA