Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makocha Simba na Yanga wavimbiana kuelekea fainali

Alhamisi , 23rd Sep , 2021

Makocha wa vilabu vya Simba na Yanga wamezungumza kwa nyakati tofauti tofauti kuhusu maandalizi ya mchezo wa fainali ya Ngao ya Hisani ya Jamii unaotaraji kuchezwa Jumamosi ya Septemba 25, 2021 kwenye dimba la Benjamin Mkapa.

Kocha wa Simba, Mfaransa Didier Gomez (kushoto) na kocha wa Yanga, Mohammed Nasreddine Nabi (kulia).

Kocha wa Simba, Didier Gomez amesema hakuna mchezo rahisi katika haya mashindano na kila timu inafanya maandalizi kusaka ushindi hivyo wanapaswa kuwa makini ili wapate matokeo mazuri huku akiwa na imani ya kushinda kombe hilo na kuanza msimu vizuri.

"Nina Imani tutaanza msimu mzuri kwa kushinda taji, tumefanya maandalizi ya kutosha wakati huu. Tumejipanga kimbinu na tumeendelea kurekebisha makosa machache, pia tumeboresha maeneo tuliyokuwa bora ili kuhakikisha tunaanza msimu kwa kuchukua taji na kama  tulivyomaliza msimu kwa kushinda mataji"

"Hakuna mechi rahisi katika haya mashindano na kila timu inafanya maandalizi kusaka ushindi, tunapaswa kuwa makini ili tupate matokeo mazuri ambayo yatatupeleka katika hatua inayofuata"

Kwa upande wa kocha wa Yanga, Mohammed Nasreddine Nabi amesema wanahitaji kushinda mechi hiyo kuliko kitu kingine kwa sasa kwasababu hawakufanya vizuri kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Afrika hivyo wameelekeza akili na mipango yote kwenye fainali hiyo na kukiri kuwa wapo tayari kuanza na rekodi nzuri katika msimu ujao.

"Tunahitaji kuahinda mechi hiyo kuliko kitu kingine kwa sasa, hatukufanya vizuri kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, sasa tumerejea kamili kwenye mashindano ya ndani, tunaanza na Ngao ya Jamii halafu akili na mipango itahamia kwenye ligi kuu Tanzania Bara"

"Tuko tayari, tunajua umuhimu wa kupata ushindi Jumamosi, tunataka kuanza na rekodi nzuri katika msimu wa mwaka 2021-22".

Mchezo huo utakuwa watatu kwa mapacha hao wa kariakoo kukutana kwenye kalenda ya mwaka 2021 baada ya kukutana Julai 3 kwenye mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi kuu na baadae Julai 25 kwenye fainali ya kombe la Shirikisho nchini huku Simba akiibuka bingwa kwa kupata ushindi wa bao 1-0 baada ya kufungwa 1-0 kwenye Ligi kuu.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava