Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mambo 5 kuelekea mechi ya Simba na Yanga

Jumapili , 12th Jul , 2020

Leo Julai 12 ni siku nyingine tena ambayo nchi itasimama kwa dakika 90 kupisha mtanange wa nguvu kati ya Simba na Yanga, awamu hii ikiwa ni katika Kombe la Shirikisho.

Simba na Yanga

Mchezo huu ni mkubwa si tu kutokana na uhasama wa timu hizi mbili, bali kwa jinsi kila timu inavyohitaji ushindi ili kufanikisha kitu fulani kikubwa katika historia yake. Yafuatayo ni mambo 5 ambayo unatakiwa kuyafahamu kuelekea mchezo huo.

Mosi: Mchezo huu ni wa tatu kuzikutanisha timu hizo msimu huu, mchezo wa kwanza uliochezwa Januari 4, 2020 ulimalizika kwa sare ya mabao 2-2, mchezo wa pili uliochezwa Machi 8, 2020 ulimalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao moja kupitia kwa Bernard Morrison.

Pili: Mchezo huu hautakuwa na mashabiki wengi zaidi kama ilivyokuwa ikitokea katika michezo ya hapo nyuma kutokana na tahadhari ya janga la Corona, ambapo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza kuwa watazamaji watakaoruhusiwa ni 30,000 pekee.

Tatu: Simba inahitaji kushinda mechi hii ili kuhalalisha kile wanachokiamini kuwa hakuna raha ya kusheherekea ubingwa bila ya kuifunga Yanga, huku Yanga ikihitaji zaidi ushindi ili kuweka matumaini ya kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao (Kombe la Shirikisho barani Afrika).

Nne: Jumla ya waamuzi 6 watahusika katika kusimamia mchezo huo wa leo, kutokana na kuwepo kwa changamoto ya maamuzi katika michezo ya hivi karibuni, ambapo waamuzi wawili watawekwa mahususi kwenye magoli yote mawili.

Tano: Tahadhari kwa timu zote mbili kutokana na matokeo yatakayopatikana kwenye mchezo wa leo hasa Yanga, kuwa endapo watapoteza mchezo huu watapoteza nafasi ya kucheza michuano ya kimataifa msimu ujao hivyo kuhatarisha vibarua vya makocha hata baadhi ya wachezaji, kwani matukio kama hayo yaliwahi kujitokeza katika mechi mbalimbali huko nyuma ambazo makocha walifukuzwa baada ya kupoteza mchezo wa watani.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu