Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Man United yaipiku Real Madrid kwa mkwanja

Alhamisi , 19th Jan , 2017

Timu ya Manchester United imepata kipato kikubwa kuliko timu yoyote katika msimu uliopita na kuipiku Real Madrid iliyokuwa kinara kwa mapato kwa takriban miaka 11

Hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na kampuni ya Deloitte ambayo ni miongoni mwa kampuni kubwa za ukaguzi duniani ambapo imeitaja Man United kuingiza paund milioni 515 (euro 689m) sawa na shilingi za kitanzania trilioni 1.6 katika msimu wa 2015/16

Hii ni mara ya kwanza kwa Man United kushikia nafasi hiyo tangu msimu wa 2003/04.

Katika taarifa hiyo, klabu hiyo ya Man United inayoshiriki ligi kuu ya England ( EPL) imeshuhudia mapato yake yakiongezeka kwa wastani wa paund milioni 71 (euro milioni 100) na kwa kiasi kikubwa ni mapato ya kibiashara.

Real Madrid waliokuwa vinara wameengiza paund milioni 463 (euro 620.1) sawa na shilingi trilioni 1.478 wameporomoka hadi nafasi ya tatu nyuma ya Barcelona walioendelea kubaki katika nafasi ya pili kwa kipato chao cha shilingi za kitanzania trilioni 1.479

Bayern Munich imepanda kutoka nafasi ya 5 hadi ya nne, huku Man City pia wakipanda kutoka nafasi ya sita hadi ya 5.

Ukijumlisha vipato vya timu ishirini bora kwa msimu wa 2015-2016 vimeongezeka kwa asilimia 12% na kufikia paund bilioni 6.41 (euro billioni 7.4) sawa na shilingi 17.7 za kitanzania kikiwa ni kiwango ambacho hakijawahi kutokea.

 

 

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji