Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara aingilia kati sakata la shabiki wa Yanga

Jumapili , 17th Feb , 2019

Baada ya kumalizika kwa mchezo wa watani wa jadi Yanga na Simba katika uwanja wa taifa, Shabiki maarufu wa Yanga, Jimmy amezua gumzo mtandaoni baada ya kutoa chozi hadharani kufuatia kichapo cha bao 1-0 ilichokipata timu yake.

Haji Manara na Jimmy akiwa na mkewe (kulia)

Jimmy ambaye mara kwa mara hushiriki katika kipindi cha Kipenga Extra cha East Africa Radio, alimwaga chozi mbele ya waandishi wa habari akisema kuwa anahofia zaidi juu ya ahadi ambazo aliziahidi kwa wapinzani wake Simba katika mchezo huo.

Aliahidi kuwa endapo Yanga ikifungwa na Simba, atamweka rehani mkewe na yeye mwenyewe kuvua nguo Kariakoo, ambapo alikuwa akiwaomba mashabiki wa Simba wamsamehe kwa ahadi zake.

Suala hilo limemuibua Afisa Habari wa Simba, Haji Manara ambaye katika ukuirasa wake wa Instagram ameandika, "ninakuombea msamaha ili mkeo anusurike!!. Simba ni watu waungwana na kwa kuwa umeomba radhi tunaamini uliyepinga nae atakusamehe pia, ila 'next time' iwe fundisho kwa wafuasi wa Mbuteni msithubutu kutoa ahadi kwa bingwa wa nchi,!".

Baada ya kutoka uwanjani na kufika nyumbani kwake, hali ya Jimmy haikuwa nzuri kwani alikuwa akilalamika mbele ya wazazi na ndugu zake lakini akishindwa kueleza nini kinamsumbua.

Katika ukurasa wa Istagram wa George David 'Kampista' ambaye ni mtangazaji wa michezo East Africa Radio, ameweka video inayoonesha hali ya shabiki huyo baada ya kufika nyumbani kwake.
 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava