Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara arudisha pesa za Yanga, aeleza kilichomkuta

Jumanne , 3rd Mar , 2020

Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara leo, Machi 3, 2020 amefika Makao Makuu ya klabu ya Yanga kwa ajili ya kurejesha pesa za matibabu alizochangiwa na mashabiki wa klabu hiyo.

Haji Manara alipokuwa makao makuu ya klabu ya Yanga

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema kuwa ameamua kubadilisha uamuzi wake baada ya kukutana na wazee wa Yanga Makao Makuu ya klabu na kumshauri kuwa asitishe mpango wake kwakuwa wao ni watani wa jadi kwa muda mrefu.

"Nilikwenda mwenyewe mchana huu klabuni Yanga,bahati mbaya sana sikuwakuta viongozi wa klabu, wazee niliowakuta nje baada ya kuwaeleza nimekuja kukabidhi pesa za masimango walinisihi sana nisifanye hivyo na wakaniambia yule ni mgeni hapa mjini na hajui tamaduni zetu na kuniomba nisirejeshe hata thumni", amesema Manara.

"Nimefundishwa kuwatii wazee, na ntarejea kwa Wanasimba walionikabidhi pesa zao, busara itawashauri tupeleke hospitali kwa wagonjwa wasiojiweza, ikiwapendeza tutafanya hvyo", ameongeza.

Hatua hiyo imekuja baada ya maoni ya mmoja wa watu maarufu ndani ya klabu ya Yanga, maoni ambayo Manara amesema hayakumpendeza yanayohusu pesa ambazo aliwahi kuchangiwa na mashabiki wa Yanga kwa ajili ya matibabu yake.

Joto la mchezo wa mahasimu hao linazidi kupanda, ambapo mchezo wao unatarajiwa kupigwa Machi 8, 2020 katika Uwanja wa Taifa, huku Yanga wakiwa wenyeji.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava