Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara atoa sababu ya kutojibu salamu za Wanayanga

Jumatatu , 21st Jan , 2019

Klabu ya soka ya Simba imerejea asubuhi ya leo kutokea mjini Kinshasa ambako ilicheza mchezo wa Klabu Bingwa Barani Afrika dhidi ya AS Vita Club.

Haji Manara

Simba imereja nyumbani ikiwa na kumbukumbu mbaya kichwani, ikipoteza mchezo huo kwa mabao 5-0.

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara ambaye amekuwa akiandamwa na mashabiki wa Yanga kutokana na tambo zake, amejitokeza na kueleza sababu ambayo imepelekea ukimya wake baada ya mchezo huo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema kuwa sababu iliyomfanya kushindwa kujibu ujumbe wa watani wake ni tatizo la mtandao nchini DR Congo.

 

Kufuatia matokeo hayo, sasa Simba inakamata nafasi ya tatu katika kundi lake la D, ikiwa na alama 3 na magoli 3. Kundi hilo linaongozwa na Al Ahly iliyo na alama 4, AS Vita iliyo nafasi ya pili kwa alama 3 na JS Saoura inayoburuza mkia kwa alama moja pekee.

Baada ya kurejea nchini, Simba itaingia moja kwa moja kambini tayari kwa maandalizi ya mashindano ya Sport Pesa Seper Cup yanayotarajia kuanza kesho katika uwanja wa taifa, kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu hiyo.

Simba inatarajia kukutana na AFC Leopards ya Kenya katika mchezo wa awali na imesema kuwa itayatumia mashindano hayo kwaajili ya kujiandaa na michuano inayoendelea ya Klabu Bingwa Afrika.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu