Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara awataka wachezaji kuchukua tahadhari

Alhamisi , 16th Mei , 2019

Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amewakumbusha wachezaji wa klabu hiyo siri ya mafanikio kuelekea katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar hii leo.

Wachezaji wa Simba

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amezungumzia umuhimu wa mchezo huo dhidi ya Mtibwa, akiufananisha na mchezo wa hatua ya 16 bora ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya AS Vita jijini Dar es salaam, ambapo amewakumbusha jinsi walivyohamasishana katika chumba cha kubadilishia nguo.

"Wachezaji wetu wapendwa, mnajua mapenzi waliyonayo Wanasimba kwenu, mnafahamu kiu yao!!, mnajua karaha wazipatazo mtaani msiposhinda mabingwa wetu wa nchi!!, najua sometimes mpira una matokeo ya kihayawani lakini nyie ni 'another level' mkidhamiria kwa jinsi nnavyowajua", amesema Manara.

"Nakumbuka mlipoambiana 'Dressing room' katika mchezo na As Vita, hebu katupeni pointi tatu leo!!, tunahitaji pointi tatu tu vijana wetu, Yes Mtibwa ni timu bora mno ila mkiamua kwa uwezo wa Mungu, nyie ni bora maradufu".

"Haya haya haya haya wanaume, Wanasimba leo watakuja kuwapa support ili tuanike makopa juani!, inshaallah kheri", ameongeza.

Simba iko katika nafasi ya pili kwa pointi 82, nyuma ya Yanga iliyo katika nafasi ya kwanza kwa pointi 83. Ratiba ya ligi kuu inatarajia kumalizika Mei 28 kwa timu zote kushuka dimbani katika viwanja tofauti tofauti.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava