Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mashabiki na viongozi walivyoigharimu AS Roma

Jumamosi , 21st Jul , 2018

Kufuatia maamuzi ya shirikisho la soka barani Ulaya UEFA kuipiga faini nyingine klabu ya AS Roma kutokana na vurugu za mashabiki na kauli tata za viongozi katika msimu wa ligi ya mabingwa Ulaya uliomalizika, tunatazama jinsi viongozi na mashabiki hao walivyoigharimu klabu yao.

Mashabiki wa AS Roma wakiisapoti timu yao katika moja ya mchezo

Mmiliki wa wa klabu ya AS Roma ya nchini Italia, James Pallotta amefungiwa miezi mitatu kuhudhuria michezo yoyote ya shirikisho la soka barani Ulaya UEFA kuanzia sasa kwa kosa la kumdharau mwamuzi.

Pallotta amepewa adhabu hiyo kufuatia kauli yake ya kumwita mwamuzi ‘kituko’ katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya kati ya AS Roma na Liverpool uliofanyika Mei, 2 mjini Roma ambapo klabu yake licha ya ushindi wa 4-2, iliondolewa katika hatua ya nusu fainali.

Katika maamuzi hayo yaliyotelewa na UEFA, pia klabu ya AS Roma imepigwa faini ya Euro 19,000 ambazo ni sawa na takribani shillingi millioni 50.4 za kitanzania kutokana na vurugu za mashabiki .

Katika mchezo wa awali wa nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya, AS Roma ilipigwa faini ya Euro 50,000 ambazo ni sawa na takribani shillingi millioni 132.6 za kitanzania kutokana na vurugu za mashabiki ambazo zilipelekea kujeruhiwa vibaya kwa shabiki mmoja wa Liverpool.

Kwenye msimu uliopita wa ligi ya mabingwa barani Ulaya, klabu ya AS Roma imetozwa jumla ya Euro 89,000 ambazo ni sawa na takribani shilling za kitanzania millioni 236.1 kutokana na vurugu za mashabiki na kauli tata za viongozi wa klabu hiyo.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine