Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meck Sadick atoa neno baada ya Tarimba kukaa kando

Jumanne , 10th Jul , 2018

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kuivusha Yanga, Meck Sadick, amesema hana taarifa rasmi za kujiuzulu kwa Mwenyekiti wake katika kamati hiyo Tarimba Abbas, bali amezisikia tu kama watu wengine.

Tarimba Abbas (kushoto) na Meck Sadick (Kulia)

Sadick ambaye ni moja ya wanachama wenye heshima ndani ya klabu hiyo, ameeleza kusikitishwa na taarifa hizo na kuahidi kumfuata Tarimba na kuongea naye binafsi ili kujua nini sababu ya yeye kukaa kando.

''Kwasasa sio wakati mzuri wa kujadili kila jambo hata kama kweli kuna wakati mgumu tunapitia, Tarimba anaweza kuwa amekasirishwa na kitu binafsi pengine nikiongea naye mimi anaweza kusema tatizo na akarudi kwenye nafasi yake ila kwasasa tusubiri kwanza'', - amesema.

Tarimba alitangaza kuachia nafasi yake jana jioni kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokuwepo kwa maelewano kati ya viongozi wa sasa wa klabu na viongozi wa kamati maalum ya kuivusha Yanga katika kipindi cha mpito ambayo yeye alikuwa anaiongoza kama Mwenyekiti.

Meck Sadick ambaye ni mkuu wa mkoa mstaafu aliyehudumu katika mikoa ya Dar es salaam na Kilimanjaro kwa vipindi tofauti, aliteuliwa kuwa makamu mwenyekiti wa kamati hiyo kupitia mkutano mkuu wa klabu uliofanyika Mei 20 huku Tarimba Abbas yeye akiteuliwa kuwa Mwenyekiti.

Tarimba ameiongoza kamati hiyo kwa siku 50, lengo kuu ikiwa ni kusaidia timu kwenye maeneo kadhaa ikiwemo usajili na maandalizi ya uchaguzi kwaajili ya kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mwenyekiti Yusuf Manji. Aidha kamati hiyo ilipata baraka za baraza la wadhamini la Yanga chini ya Mwenyekiti George Mkuchika ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala bora.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava