Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miyeyusho ayeyushwa kwa KO huko Jamhuri ya Czech

Jumatatu , 4th Jul , 2016

Ile desturi ya mabondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania kutofanya vema nje ya nchi katika mapigano yao ya kirafiki na kimashindano imeendelea tena mara baada ya bondia Francis Miyeyusho naye kupoteza pambano la ubingwa wa UBO ugenini nchini Czech

Bondia Francis Miyeyusho 'chichi mawe'.

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania Mtanzania Francis Miyeyusho maarufu kama 'Chichi Mawe' mwishoni mwa juma lililopita alishindwa kuipeperusha vema bendera ya taifa baada ya kupoteza mpambano wake wa kimataifa wa raundi 12 kuwania ubingwa wa mabara wa UBO International akipambana na bondia toka nchini Czech.

Miyeyusho ambaye ni mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam alipoteza mpambano huo baada ya kupigwa kwa technical knock out (KO) na mpinzani wake Martin Parlagi katika mpambano uliopigwa mjini Plague Jamhuri ya Czech.

Kwa mujibu wa mratibu wa ndani wa mpambano huo katibu mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) Antony Rutha amesema bondia huyo 'Chichi Mawe' alipoteza mpambano huo mapema katika raundi ya pili tu mara baada ya kupigwa ngumi ya tumbo na kujikuta akishindwa kuendelea na mpambano huo baada ya kuhisi maumivu makali ya tumbo na hivyo kumlazimisha mwamuzi kusimamisha mpambano huo na kumpa ushindi bondia Martin Parlag na kutwaa mkanda huo wa UBO kwa Mabara.

Kipigo hicho kinakuwa ni moja ya mwendelezo wa mabandia wengi wa ngumi za kulipwa nchini kushindwa kutamba katika mapambano wakiwa ugenini na kimsingi wadau wa ngumi wakiwemo mabondia wenyewe na viongozi wao na makocha wanatakiwa kujiuliza wapi wanajikwaa ama wanaangukia na kujikuta wakishindwa kufua dafu katika mchezo huo wakiwa ugenini.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa