Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Morrison siyo mkubwa kuliko Yanga" - Katibu

Ijumaa , 19th Jun , 2020

Uongozi wa klabu ya soka ya Yanga umesema hauna nia ya kumtukuza mchezaji kutokana na ubora wake kwa kuwa taasisi ya klabu hiyo ni kubwa kuliko mtu yoyote.

Bernard Morrison akimtoka mchezaji wa wa Transit Camp

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Wakili Patrick Simon akizungumzia adhabu walizotoa dhidi ya nyota wao wa kigeni Lamine Moro aliyeonesha utovu wa nidhamu katika mechi dhidi ya JKT Tanzania, na Benard Morrison aliyeshindwa kusafiri na klabu katika mikoa ya Shinyanga na Dodoma.

Akizungumza na Kipenga ya East Africa Radio kinachoruka kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa saa mbili usiku, Wakili Patrick amesema Yanga haiungi mkono mchezo hatarishi kwa kuwa mpira wa miguu sio vita, pia haijafurahia kumkosa Lamine Moro katika mechi tatu zijazo kwa kuwa kunaweza kuigharimu timu.

Simon Patrick amesema klabu imemuadhibu nyota huyo kutokana na kanuni na sheria zilizopo, ingawa amesisiza kuwa hafahamu kama viongozi waliopita walikua wanatoa adhabu kwa wachezaji wengine waliokiuka kanuni zilizowekwa.

Kuhusiana na Bernard Morrison, Wakili Patrick amesema alizungumza naye na alimsamehe kwa kuwa alikua na hoja za msingi lakini amesisitiza kwamba maamuzi ya kumsamehe si kutokana na hadhi yake.

Amesema "Morrison ni mchezaji wa kawaida kama wachezaji wengine, Yanga ni kubwa kuliko yeye na hakuna aliyemfahamu mchezaji huyo wa Ghana kabla ya kusajiliwa na klabu yetu"

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava