Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mshahara wamuondoa Ramos Madrid

Alhamisi , 17th Jun , 2021

Klabu ya Real Madrid imethibitisha kuwa itaachana na nahodha wake Sergio Ramos pindi mkataba wake na klabu hiyo utakapo malizika mwishoni mwa mwezi huu, baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka 16.

Sergio Ramos

Ramos anaondoka Madrid baada ya kushindwa kufikia makubaliano ya kusaini mkataba mpya, ambapo Ramos alikuwa anahihitaji mkataba wa miaka miwili na ongezeko la mshahara, wakati klabu ilimpa ofa ya mkataba wa mwaka mmoja na punguzo la asilimia 10 kutoka kwenye mshahara wake wa sasa, hivyo wakafikia muafaka wa kutosaini mkataba mpya kutokana na kutofautiana kwenye vipengele hivyo.

Mlinzi huyo wa kati mwenye umri wa miaka 35 alijiunga na Madrid mwaka 2005 akitokea Sevilla na ameshinda jumla ya mataji 22 akiwa na Los Blancos ambapo ametwaa ubingwa wa Ligi Kuu La Liga mara 5 na ubingwa wa klabu bingwa ulaya mara 4.

Msimu wa 2020-21 haukuwa mzuri kwa Ramos kwani aliandamwa na majeruhi ya mara kwa mara ambayo yamemsababishia kutojumuhishwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Hispania kinachoshiriki michuano ya Euro 2020 inayoendelea. Ndani ya msimu huo alicheza michezo 21 ikiwa ni idadi ndogo zaidi tangu ajiunge na klabu hiyo.

Vilabu vya PSG ya Ufaransa na klabu yake ya zamani ya Sevilla ndio vinatajwa kuonyesha nia ya kuhitaji huduma ya Ramos.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava