Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Neno la Mkwasa alipokutana na wachezaji Yanga

Jumatano , 6th Nov , 2019

Kocha mpya wa klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa amezungumza kwa mara ya kwanza na wachezaji wa klabu hiyo baada ya kuteuliwa jana, Novemba 5.

Kocha Charles Boniface Mkwasa na baadhi ya wachezaji wa Yanga.

Mkwasa ambaye aliwahi kuifundisha klabu hiyo kwa vipindi vitatu tofauti, amerejea baada ya uongozi kumfuta kazi kocha Mkongo, Mwinyi Zahera pamoja na benchi lake la ufundi.

Akizungumza mbele ya wachezaji hao, Mkwasa amesema, "lengo la kwanza la kila mchezaji anaekuja hapa ni kuhakikisha Yanga inabeba ubingwa. Ni lazima tuanze kushinda mechi zetu."

"Hamtachukiwa na mashabiki kama mtacheza vizuri na kushinda. Maisha yenu yatakua mazuri sana. Watu watakuja viwanjani na mtalipwa kwa wakati, nyie ni wachezaji wazuri sana na mimi niko hapa kuwasaidia kulifanikisha hilo.", ameongeza Mkwasa .

Charles Boniface Mkwasa sio mgeni katika klabu ya Yanga, alianza kuichezea klabu hiyo mwaka 1979 akitokea Mseto ya Morogoro na  alikuwa nahodha wa Yanga kuanzia mwaka 1986 hadi 1989 alipostaafu.

Mwaka 1991 alirudi kuwa kocha msaidizi chini ya kocha Syllersaid Mziray hadi mwaka 1993 na kuondoka. Alirejea tena mwaka 2001 ambapo alikuwa kocha mkuu wa Yanga hadi 2002 kabla ya kuondoka kwa mara ya pili kama kocha. Baada ya hapo alirudi mwaka 2013 kama kocha msaidizi wa Hans van der Pluijm hadi mwaka 2015.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava