Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nigeria wamuumiza kichwa Zitto, atamani wengine

Jumatatu , 20th Mei , 2019

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amempongeza nahodha wa taifa Stars Mbwana Samatta, kwa kutwaa ubingwa wa soka Ubelgiji na klabu yake ya KRC Genk.

Zitto Kabwe

Zitto ambaye ni shabiki mkubwa wa soka akishabikia klabu za Simba na Liverpool amesema, Tanzania inahitaji watu kama Samatta wengine 100 ili kusaidia kulitangaza taifa letu kimataifa.

Zitto ametumia Instagram kueleza hayo akiweka wazi kuwa video ya mashabiki wa Genk wakishangilia na bendera ya Tanzania ni kitu kikubwa kwa taifa. ''Hii ni free advert ya nchi. Hapa ni Genk ambapo @samagoal77 anacheza. We need hundreds of Samatta nje''.

Aidha Zitto ameeleza namna ambavyo Nigeria inapata faida kama hizo kutokana na kuwa na wachezaji wengi Ulaya. ''Fikiria Nigeria wanapata Remittances kiasi gani kutoka exports ya wachezaji wao kwenye ligi za Ulaya na penginepo.

Mashabiki wa Genk na Samatta wakipeperusha bendera ya Tanzania kwenye uwanja wa Cristal Arena.

Pia amemshukuru Samatta kwa kusema ''Asante sana Mbwana Samatta kwa heshima hii kwa nchi yetu''.

Samatta akiwa na Genk amefanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya huko huku akimaliza akiwa kinara wa magoli baada ya kufunga mabao 20 kwenye msimu wa 2018/19.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto