Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyota wa Sprite Bball Kings aenda Afrika Kusini

Jumatatu , 30th Jul , 2018

Mchezaji kutoka timu ya Kikapu ya Portland inayoshiriki michuano ya Sprirte Bball Kings Ally Atiki ameondoka leo Julai 29, kuelekea nchini Afrika Kusini kushiriki kambi ya mafunzo ya mchezo huo, inayojulikana kama Basketball Without Borders (BWB).

Kikosi cha Portland na aliyewekewa kiboma chekundu ndio Ally Atiki

Kambi hiyo itakayofanyika jijini Pretoria itaanza Jumatano Agosti 1 na kukamilika Agosti 4 na itaendeshwa na wachezaji wa Kikapu kutoka mataifa ya Ulaya na Marekani wanaocheza ligi ya Kikapu ya Marekani.

Katika safari hiyo Atiki pia ataambatana na mchezaji wa kike wa Kikapu Jesca Ngisaise Onga'anyi, Kocha wa timu ya Taifa ya Vijana Bahati Mgunda na viongozi wa Shirikisho la Kikapu nchini (TBF) Rais Phares Magesa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es salaam (BD) Okare Emesu.

Mbali na kambi hiyo, pia kutakuwa na mchezo wa NBA Africa 2018, ambao utakutanisha timu za Team Africa dhidi ya Team World, na utafanyika August 4 saa 11 jioni, Sun Arena, Time Square.

Ally Atiki jana Julai 29, alikuwa dimbani kwenye uwanja wa taifa wa ndani na timu yake ya Portland kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza kati ya tatu za 'Best of three' ambapo timu yake ilikubali kichapo cha pointi 70 kwa 54. 

Mechi za pili za nusu fainali zitapigwa Jumamosi ijayo Agosti 4 kwenye uwanja wa taifa wa ndani ambapo Flying Dribblers wanahitaji ushindi tu dhidi ya Team Kiza ili kutinga hatua ya fainali baada ya kushinda mechi ya kwanza kwa pointi 84 kwa 75.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava