Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sababu ya Makambo kutoonekana uwanjani

Jumatatu , 24th Sep , 2018

Uongozi wa klabu ya Yanga umekanusha uwepo wa taarifa za majeraha ya mshambuliaji wake, Heritier Makambo kufuatia kutopangwa katika mchezo dhidi ya Singida United wikiendi iliyopita.

Mshambuliaji wa Yanga, Heritier Makambo.

Mshambuliaji huyo hakupangwa katika listi ya kikosi cha kwanza cha mchezo huo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa 2-0, kulikopelekea kuzuka kwa taarifa juu ya majeraha yake na kuwa anaweza kukosekana katika mchezo dhidi ya watani wao wa jadi Simba utakaopigwa wikiendi hii.

Akizungumza na www.eatv.tv juu ya ukweli wa taarifa hiyo , Afisa habari wa Yanga, Dismas Ten amesema,

"Ni kweli Makambo hakucheza na si lazima acheze mechi zote, kiujumla yuko vizuri hana tatizo lolote na anafanya mazoezi kama kawaida", amesema Ten.

"Kucheza na kupumzika kwa mchezaji ni jambo la kawaida tuu kwasababu yeye naye ni binadamu kama wengine ambao huwa wakichoka wanapumzika hawafanyi kazi. Na kwenye hili wala asisemwe kocha kwasababu hiyo ni kawaida,  hata waliocheza jana ni wachezaji wa Yanga, yeye atacheza kwenye michezo inayofuata ", ameongeza Dismas.

Yanga itapambana na watani wao Simba, 30 Septemba katika ligi kuu Tanzania bara, mchezo ambao tayari umekwishaanza kuzua gumzo miongoni mwa mashabiki wa soka hasa wa timu hizo.

Ushindani mkubwa katika mchezo huo unatarajiwa kuwa katika kuwania nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi ambapo mpaka sasa Yanga inaongoza kwa alama 12 katika michezo yake minne huku Simba ikiwa katika nafasi ya tatu kwa alama zake 10 baada ya kushuka dimbani mara tano.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu