Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sept.1 Mfaume, Pialali kurudiana

Alhamisi , 16th Mar , 2023

Mabondia wawili mahasimu, Iddy Pialali na Mfaume Mfaume leo wamesaini mkataba wa kurudiwa kwa pambano lao linalotarajiwa kufanyika Septemba Mosi, mwaka huu, tukio lililofanyika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam huku kila mmoja akitamba kumaliza pambano mapema.

Pambano hilo lililopewa jina la King Of The Night linaloteka hisia za wengi kutokana na upinzani uliopo baina yao na kambi zao, linarudiwa baada ya lile la awali lililopigwa Arusha kuvunjika baada ya kutafsiriwa mabondia hao waligongana vichwa vilivyopelekea Pialali kupasuka usoni.

Pambano hilo lililokuwa la raundi 10 lililopigwa Desemba 26, mwaka jana na lilivunjika raundi ya kwanza.

Hata hivyo mara baada ya kuingia mkataba huo, Mfaume alitamba kuwa atahakikisha anamchakaza mpinzani wake na kama haitakuwa hivyo basi ataacha mchezo wa ngumi.

“Tusiangalie yaliyopita ilikuwaje, Watanzania wote waliona kilichotokea, hakuna kichwa ni uoga tu, sasa siku hiyo kukimbia hakuna. Mama Mfaume amesema mwanangu ‘kaza buti’.

“Tangu niko mdogo, mama yangu ananiambia hivyo, maana yake pambana, fanya mazoezi kwa bidii halafu kasema raundi ya tatu mwisho, Bi Mkubwa nimenuukuu kauli yako, huyu asipoamkia ICU (chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum), naacha boxing.

“Mama Mfaume kaongea na timu yangu timu ya Mabibo siongei sana, nasemaje tupigane mpaka mmoja afe,” alisema Mfaume.

Naye Pialali alisema: “Mapepe, muoga anatetemeka tetemeka, mwanaume anaongea sana? Mwanaume haongei sana. Nasema niko, safi niko salama, Mfaume safari hii kazi anayo, huyu (Mfaume) ni kondoo sio bondia sasa huyu kondoo dawa yake nishaipata tayari, kuna watu anawategemea lakini huyu kondoo nampiga ‘KnockOut’ mbaya sababu sio bondia, hamalizi huyu hana maajabu.

“Mfaume kampiga nani hapa Tanzania? Sisi tunacheza ngumi hatuogopi, kazi anayo, Manzese msiwe na presha, hapa anajikaza tu ila tutampiga,” alisema Pialali.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava