Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Steve Bruce kuvunja uteja kwa Arsenal leo?

Jumatatu , 18th Jan , 2021

Ligi kuu nchini England inatazamiwa kuendelea usiku wa leo tarehe 18 Januari 2021 kwa mchezo mmoja, 'Washika mitutu wa jiji la London' klabu ya Arsenal itawakaribisha Newcastle United inayonolewa na kocha Steve Bruce mchezo utakaochezwa sa 4:00 usiku leo kwenye dimba la Emirates.

Kocha wa klabu ya Newcastle United, Steve Bruce.

Kuelekea kwenye mchezo huo, Arsenal itamkosa mlinzi wake wa kati Pablo Mari ambaye anasumbuliwa na maumivu ya misuli ya nyuma ya goti aliyoyapata kwenye mchezo uliopita dhidi ya Crystal Palace na kumfanya afanyiwe mabadiliko baada ya maumivu kumzidia.

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amesema kuna hati hati kama mlinzi wake wa kushoto Kieran Tierney anayesumbuliwa na maumivu ya misuli na mshambuliaji wake Gabriel Martinelli mwenye maumivu kwenye kifundo chake cha mguu kama wataweza kucheza kwenye mchezo huo.

Taarifa nzuri kwa washika mitutu hao wa jiji la London ni kwamba, kiungo wake mpya Thomas Partey aliyesajiliwa dirisha kubwa la usajili lililopita anatazamiwa kurejea dimbani baada ya kupona maumivu  kwenye kifundo chake cha mguu na mlinzi Gabriel Magalhaes kuripitiwa kuwa fiti kuwavaa Newcastle

Kwa upande Newcastle United inayonolewa na kocha Steve Bruce, itamkosa winga wake Ryan Fraser anayetumikia aadhabu ya kukosa mchezo mmoja baada ya kuoneshwa kadi mbili za njano kwenye mchezo uliopita na kiungo Jonjo Shevley atakosekana baada ya kufanyiwa upasuaji wa paja.

Walinzi wa kati na nahodha wa Newcastle Jamal Lascelles na nahodha msaidizi Federico Fernandez hawana uhakika wa kuwemo kikosini baada ya kukutwa na Covid-19 hivyo watasubiri majibu ya vipimo vya mwisho kuonesha kama wapo fiti ama laa.

(Kwenye picha: Ni kiungo mshambuliaji wa Arsenal, Eddie Smith Rowe akipiga mpira na kuifungia Arsenal bao la pili kwenye ushindi wa Arsenal wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle kwenye kombe la FA siku tisa zilizopita.)

Mchezo huo ni fumbo kwa kocha wa Newcastle United Steve Bruce kutokana na rekodi yake mbaya mbele ya Arsenal kwenye dimba la Emirates ambapo amecheza michezo 11 dhidi ya Arsenal na kufungwa michezo 8 na kuambuliwa sare tatu bili ushindi akiwa ugenini dhidi ya Arsenal.

Leo wafuatiliaji wa soka Ulimwenguni watasubiri kuona kama kocha huyo atavunja uteja akiwa ugenini mbele ya Arsenal baada ya mchezo kumalizika. Kwa upande wa Arsenal na wenyewe hawana rekodi nzuri kwenye dimba lao hilo msimuu, wamecheza michezo 8 lakini wameshinda mchezo 1 tu.

Kwa rekodi hiyo, maana yake Arsenal wameambulia alama 5 kati ya 21 zilizotarajiwa kama wangepata ushindi kwenye michezo 7 waliyocheza na badala yake kushinda mchezo 1 pekee, kutoa sare 2 na kufungwa michezo 4 kwenye dimba la Emirates kwenye EPL msimu huu.

Arsenal ambaye wameifunga Newcastle mabao 2-0 siku 9 zilizopita na kuwatoa kwenye mzunguko wa tatu wa kombe la FA, huenda wakiingia kifua mbele na rekodi yao nzuri mbele ya Newcastle ya kuwafunga mara 14 kwenye michezo 15 ya mwisho waliyocheza tokea wafungwe 2010 bao 1-0.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava