Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Suala la mavazi ya Zahera' lafika Bungeni

Jumatano , 4th Sep , 2019

Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abdallah Mtolea, amehojia kanuni za shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kukagua mavazi ya Makocha wa timu za Ligi, huku kukiwa na kundi kubwa la wachezaji ambao hawana bima.

Mbunge Mtolea amehoji suala hilo Bungeni, wakati akiuliza swali kwenda kwa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, juu ya malalamiko ya wachezaji wengi kukosa uhakika wa kupata matibabu kwenye timu zao.

"Wachezaji wengi hawana bima ya Afya, Serikali iko tayari kulishauri Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liachane na kuchunguza makocha wamevaa nini, bali wawatafutie wachezaji bima." amehoji Mtolea.

Akijibu swali hilo Bungeni, Naibu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Mh. Juliana Shonza amesema watahakikisha wanawashinikiza TFF kulishughulikia suala hilo kwa haraka.

"Kama Wizara tumepokea ushauri, tutaishauri TFF kuhusu bima kwa wachezaji, lakini kuhusu bima za Afya ni jambo la msingi kwa Watanzania wote." amejibu Juliana Shonza.

Mapema jana Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, lilitoa taarifa kumfungia mechi tatu kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera, kwa kukiuka kanuni za mavazi kwenye ligi.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu