Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yapanda viwango FIFA.

Alhamisi , 21st Oct , 2021

Tanzania imepanda kwa nafasi mbili katika viwango vya ubora wa soka kwa mwezi Oktoba vilivyowekwa hadharani leo na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA).

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichocheza dhidi ya Benin Oktoba 7, 2021.

Kutoka nafasi ya 132 iliyokuwepo katika viwango vya mwezi Septemba, Tanzania imesogea hadi nafasi ya 130 katika orodha ya viwango vipya ambayo FIFA wameitoa leo, Alhamisi, Oktoba 21.

Ushindi wa bao 1-0 ambao Tanzania iliupata dhidi ya Benin katika mechi ya hatua ya makundi ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia kwa upande wa bara la Afrika, Oktoba 10 umeonekana kuchangia kwa kiasi kikubwa Tanzania kupanda kwa nafasi hizo mbili.

Tanzania imepanda hadi nafasi hiyo ya 132 baada ya kufikisha jumla ya pointi 1123.84 kutoka zile 1115.37 ilizokuwa nazo mwezi uliopita.

Wakati Tanzania ikipanda, majirani zake wa Afrika Mashariki, Kenya wameporomoka kwa nafasi mbili kutoka ile ya 102 waliyokuwepo awali hadi nafasi ya 104 ambayo wameangukia kwa viwango vya mwezi Oktoba.

Rwanda imeanguka kwa nafasi tano kutoka ile ya 128 hadi nafasi ya 133 wakati Burundi imebaki katika nafasi ya 141 iliyokuwepo hapo awali.

Uganda imeendelea kuwa kinara kwa upande wa ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kupanda kwa nafasi nne kutoka ile ya 86 hadi nafasi ya 82 mtawalia

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava