Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tarehe ya Zana Coulibaly kucheza Simba yajulikana

Jumapili , 9th Dec , 2018

Ni rasmi sasa, muda ambao mlinzi mpya wa klabu ya Simba, Zana Coulibaly ataanza kuonekana uwanjani umejulikana kwa mujibu wa kocha mkuu wa 'Wekundu hao wa Msimbazi, Patrick Aussems.

Mchezaji, Zana Coulibaly (kushoto), Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori (katikati) na Kocha, Patrick Aussems (kulia).

Mlinzi huyo raia wa Burkina Faso alisajiliwa mapema mwezi uliopita akitokea klabu ya Asec Mimosas ya Ivory Coast kwa lengo la kuisaidia klabu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Klabu Bingwa barani Afrika baada ya kuumia kwa beki Shomari Kapombe.

Akizungumza juu ya muda wa mchezaji huyo kuanza kuichezea Simba, Aussems amesema kuwa hatoitumikia Simba katika michuano ya kimataifa mpaka pale watakapofanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa barani Afrika kutokana na kuzuiwa kuingiza majina mapya katika hatua za awali.

"Siwezi kumtumia hivi sasa katika michuano ya kimataifa kutokana na sheria kutubana, lakini tukitinga hatua ya makundi nitaanza kumtumia," amesema Aussems.

"Huku kwenye ligi watu wataanza kumuona katika mzunguko wa pili kwa sababu hapo atakuwa fiti zaidi na naamini atakuwa msaada mkubwa kwenye timu na kuziba pengo la Kapombe," ameongeza.

Simba hivi sasa inajiandaa kwaajili ya mchezo wa hatua ya pili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Nkana FC ya Zambia, Disemba 15, mchezo ambao Simba itaanzia ugenini nchini humo.

Pia katika kuelekea mchezo huo, klabu ya Simba imetoa nafasi kwa mashabiki wake wanaotaka kwenda kuishangilia timu yao nchini Zambia, ambapo jumla ya nauli ya kwenda na kurudi ikiwa ni Sh 130,000. Msafara ukitarajiwa kuanza Alhamisi ya wiki ijayo na kufika nchini Zambia Ijumaa, siku moja kabla ya mchezo huo utakaopigwa Jumamosi.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe