Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TFF yakemea vikali kauli za ubaguzi kwenye soka

Alhamisi , 3rd Dec , 2020

Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) limekemea kauli zenye lengo la kuzuia haki ya mashabiki kuingia viwanjani.

Taarifa hiyo ya TFF imesainiwa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo

Taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo inasema,

“Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) linakemea kwa nguvu kauli zenye lengo la kuzuia haki ya washabiki kuingia viwanjani.”

Taarifa hiyo ikasisitiza kuwa, “kwa mujibu wa katiba ya shirikisho la kimataifa la mpira wa miguu FIFA na ile ya TFF, vitendo vya aina yoyote ya ubaguzi havikubaliki katika mpira wa miguu. Hivyo mshabiki yeyote anaruhusiwa kuingia kwenye mechi ya mpira wa miguu nchini ikiwa tu havunji sheria na taratibu za mpira wa miguu ambazo zimeainishwa kupitia katiba na kanuni husika''.

Taarifa hiyo ilimaliza kwa kusema, ''Hata klabu ambazo zinamiliki viwanja, hutenga tiketi maalum kwa ajili ya timu pinzani na makundi maalum.”

Taarifa hii ya TFF imekuja baada ya hapo jana Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Haji Manara, kusema kuwa mchezo wao wa kimataifa wa klabu bingwa Afrika wa hatua ya awali wa mkondo wa pili dhidi ya Plateau United ya Nigeria, kuwa mashabiki wa klabu hiyo pekee ndio wanapaswa kuingia uwanjani kwenye mchezo huo na mashabiki wa timu nyingine tofauti na Simba SC wasijitokeze kwenye mchezo huo.

Kauli ya Manara imezua mijadala miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka wakiamini kauli hiyo inaweza, kusababisha migogoro au vurugu miongoni mwa mashabiki endapo kama mashaki tofauti na wale wa klabu ya Simba watajitokeza katika mchezo huo.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava