Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tuzo ya Mkwasa ya kocha bora VPL yazua mzozo

Jumatano , 8th Jan , 2020

Jana Januari 7, 2020 Shirikisho la Soka Tanzania TFF limetoa tuzo ya kocha bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mwezi Disemba pamoja na tuzo ya mchezaji bora wa mwezi kwa mwezi huo.

Kocha bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara mwezi Disemba, Charles Mkwasa.

Tuzo ya mchezaji bora imekwenda kwa kiungo wa klabu ya Simba, Francis Kahata akiwashinda Hassan Dilunga wa Simba na Bakari Mwanyeto wa Coastal Union alioingia nao fainali, huku tuzo ya kocha bora wa VPL kwa mwezi Disemba ikienda kwa kocha wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa, akiwashinda Juma Mgunda wa Coastal Union na Sven Vandenbroeck wa Simba.

Kipengele cha kocha bora wa mwezi kimeonekana kuzua sintofahamu baada ya kulalamikiwa na wadau wengi wa soka, ambao wanasema kuwa kocha Mkwasa hakustahili kushinda tuzo hiyo mbele ya kocha wa Simba na Coastal Union ambao walifanya vizuri zaidi yake kwenye mwezi huo.

Yanga imecheza mechi tatu mwezi Disemba, ikishinda mechi mbili ambazo ni dhidi ya Tanzania Prisons (1-0) na Biashara United (1-0) huku ikitoa sare na Mbeya City, Simba pia ikicheza mechi tatu na kufanikiwa kushinda mechi zote tatu ambazo ni dhidi ya Ndanda FC (2-0), KMC (2-0) na Lipuli FC (4-0).

Coastal Union nayo imecheza mechi tatu mwezi Disemba, ikishinda mechi zote tatu dhidi ya Mbeya City 1-0, Azam FC 1-0 na Tanzania Prisons 2-0.

Afisa habari wa Simba, Haji Manara ni mmoja ya ambao hawajaridhishwa na tuzo hiyo kupewa kocha Mkwasa, ambapo amesema, "Mkwasa hakustahili kushinda hii tuzo kwa mwezi Disemba, kacheza mechi tatu, Mbeya City 0-0, Prisons kashinda 1-0 na akashinda 1-0 dhidi ya Biashara. Kocha wa Simba naye kacheza mechi tatu zote kashinda tena kwa magoli mengi zaidi, 4-0 na Lipuli, 2-0 dhidi ya Ndanda na KMC lakini hata kocha wa Coastal Union, Juma Mgunda kafanya vizuri kuliko Mkwasa".

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava