Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vita ya 31 kwa Azam na Simba tofauti yao ni 1 tu

Jumatatu , 13th Mei , 2019

Kuelekea mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara kati ya Simba SC dhidi ya Azam FC leo Mei 13, 2019, timu hizo zinatawaliwa na rekodi mbalimbali lakini kubwa ni katika mechi za ligi kuu.

Kushoto ni John Bocco na kulia ni Salum Abubakar Sure Boys

Timu hizo zimekutana mara 30 katika michuano yote hivyo leo itakuwa ni mechi au vita ya 31 kwao, ambayo pia inaweza kuamua mbio za ubingwa kwa Simba endapo watashinda.

Katika ligi kuu timu hizo zinakutana kwa mara ya 21 ambapo mara ya kwanza ilikuwa Oktoba 4, 2008, Azam wakiwa wamepanda daraja lakini walishinda magoli 2-0 yaliyofungwa na Jamal Mnyate na Shekhan Rashid.

Katika mechi 20 zilizopita za ligi kuu, Simba wanaongoza kwa kushinda mechi 10 huku Azam FC wakishinda mechi 5 pekee na kutoka sara mara 5. Kwa ujumla zimekutana mara 30 ambapo Simba wameshinda mara 13 na Azam mara 12 huku zikitoka sare mara 5.

Tofauti kubwa katika mchezo wa leo ni kwamba wachezaji John Bocco na Salum Abubakar maarufu (Sure Boy), ndio wachezaji pekee waliokuwepo kwenye mechi ya kwanza mwaka 2008 na leo Bocco yupo Simba wakati Sure Boy bado yupo Azam FC.

Mechi inachezwa leo kwenye uwanja wa Uhuru Dar es salaam ambapo Simba ni mwenyeji. Itaanza saa 10:00 jioni. Simba ina pointi 81 kileleni wakati Azam FC ina pointi 68 katika nafasi ya 3.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa