Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachezaji Simba kujazwa noti taifa

Jumapili , 16th Dec , 2018

Inaelezwa kuwa wachezaji wa Simba wameahidiwa bonasi kubwa zaidi ya pesa na uongozi wa klabu endapo watafanikiwa kuwaondoa Nkana Red Devils kwa kupata ushindi katika mchezo wa marudiano Jijini Dar es salaam.

Simba

Pia katika hatua nyingine, kocha wa timu hiyo, Patrick Aussems amewapatia uongozi wa Simba chini ya mwekezaji Mohamed Dewji 'MO', muongozo wa kutoa pesa kwa wachezaji kama bonasi kila wanaposhinda au kusuluhu lakini pesa hizo zitatofautiana na uzito wa mashindano husika.

Mastaa hao wa Simba wanaposhinda kila mechi ya ligi kuu hupata pesa, ila kwa mechi za kimataifa mzigo ndio huwa mkubwa zaidi kuliko mechi zamichuano ya nyumbani.

Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori, bonasi wanayowapa wachezaji wao ni pesa ya kutosha na kusisitiza kuwa pesa hiyo itazidi kuongezeka kadri timu itavyozidi kusonga mbele katika mashindano hayo ya kimataifa.

Simba imepoteza mchezo wa mkondo wa kwanza kwa mabao 2-1 dhidi ya Nkana Red Devils nchini Zambia, ambapo inatarajia kurejea leo nchini tayari kwa maandalizi ya mchezo wa marudio utaopigwa wiki ijayo Jijini Dar es salaam.

Inahitaji kupata ushindi wa bao 1-0 au zaidi ili iweze kuwaondoa Nkana na kusonga mbele katika hatua inayofuata ya makundi ya michuano hiyo mikubwa zaidi barani Afrika kwa ngazi ya klabu.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine