Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wavu vyuo Vikuu Dar kupigwa April 2 mwaka huu.

Jumanne , 22nd Mar , 2016

Chama cha mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam DAREVA kinataraji kuendelea na programu za mashindano kwa kasi ile ile kama mikakati yao waliyojiwekea msimu huu katika kalenda ya matukio ya chama hicho kwa mwaka huu.

Baadhi ya wachezaji wa mpira wa wavu wakichuana katika moja ya michezo yao ya ligi ya mkoa.

Chama cha Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam kinataraji kuendelea na mipango yake ya kimashindano mwezi ujao wakati watakapoendesha ligi ya mpira wa wavu kwa vyuo vikuu itakayoanza April 2 mwaka huu na baadae kufuatiwa na ligi ndefu ya mkoa itakayoanza April 16.

Katibu mkuu wa chama cha Mpira wa Wavu mkoa wa Dar es Salaam DAREVA Yusuph Mkarambati amesema tayari wameshaanza maandalizi ya mashindano ya vyuo vikuu ambayo safari hii kwa mara ya kwanza yatakuwa yakifanyika katika viwanja vya vyuo vyote shiriki vitakavyoshiriki mashindano hayo.

Mkarambati amesema wamefikia uamuzi huo wakupeleka mashindano hayo katika vyuo husika ama shiriki kwa lengo la kuutangaza mchezo kwa watu wengine hasa jumuiya ya wanavyuo hivyo na kuwavutia kuupenda mchezo huo na pia kubwa kuongeza ushindani kwa timu shiriki kwakuwa kila timu itakuwa ikicheza vizuri ili iweze kushinda mchezo wa nyumbani mbele ya mashabiki wake.

Akimalizia Mkarambati amesema ligi hiyo ya vyuo vikuu itakayoanza April 2 mwaka huu itakuwa ni ligi fupi yenye timu nane za vyuo vikuu kutoka jijini Dar es Salaam ambayo baadae sasa itafuatiwa na ligi ndefu ya klabu bingwa ya mkoa itakayoanza kuanzia April 16 mwaka huu hadi mwezi August mwaa huu ikishirikisha vilabu takribani 12 vitakavyochuana kusaka ubingwa wa mkoa huku pia wachezaji wakiwania nafasi yakuteuliwa kuunda kikosi cha timu ya mkoa itakayoshiriki mashindano mbalimbali ya ndani na nje katika medani ya kitaifa na kimataifa kama Ubingwa wa taifa na mashindano ya majiji.

HABARI ZAIDI

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi