Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yaacha saba safari ya Majimaji

Jumapili , 15th Jan , 2017

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara Yanga SC wanaondoka leo kwenda Songea tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu siku ya Jumanne katika dimba la Majimaji Songea huku ikiacha wachezaji 7 kwa sababu tofauti.

Donald Ngoma

Mshambuliaji hatari wa timu hiyo Mzimbabwe Donald Ngoma na Wazambia Justin Zulu na Obrey Chirwa ni kati ya wachezaji saba ambao hawatakuwamo safarini.

Kaimu katibu mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit amesema kwamba watatu hao wote bado ni majeruhi na wanaendelea na matibabu.

Baraka amesema kwamba winga Emmanuel Martin yeye hatakuwamo safarini kwa sababu yuko kwenye msiba wa mdogo wake  jijini Tanga, huku Vincent Bossou yupo na timu yake ya taifa, Togo kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Gabon, wakati mshambuliaji Malimi Busungu anaachwa kwa sababu hayupo fiti. 

Kwa mujibu wa Baraka benchi la ufundi la timu hiyo chini ya kocha Mzambia, George Lwandamina linataraji kuondoka na kikosi cha wachezaji 20 tu kwenye mchezo huo kikiongozwa na makipa; Deo Munishi ‘Dida’ na Benno Kakolanya, mabeki Hassan Kessy, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Oscar Joshua, Andrew Vincent ‘Dante’, Pato Ngonyani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kevin Yondan.

Viungo ni Said Juma ‘Makapu’, Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Juma Mahadhi, Deus Kaseke, Simon Msuva, Yussuf Mhilu, Geoffrey Mwashiuya na washambuliaji Amissi Tambwe na Matheo Anthony. 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava