Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga 'yalambwa 4G' Kombe la Mapinduzi

Jumapili , 8th Jan , 2017

Timu ya Yanga leo imeangukia pua baada ya kulambwa mara nne na wana lambalamba Azam FC katika michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea Zanzibar.

Yanga na Azam katika moja ya mechi za Kombe la Mapinduzi mwaka jana

Katika mchezo huo ambao ni wa mwisho katika kundi A, Azam walianza mapema kuonesha dalili za ushindi pale ambapo nahodha wao John Bocco alipofungulia bomba kwa kumalizia mpira uliotemwa na kipa wa Yanga Deo Munisi kutokana na shuti la Sure Boy, na kufanikiwa kuandika bao la pili ikiwa ni dakika ya 2 ya mchezo.

Hadi mapumziko Azam walionekana kuutawala zaidi mchezo na kumaliza kipindi cha kwanza ikiwa na umiliki wa zaidi ya asilimia 50 huku ikishindwa kutumia nafasi kadhaa za wazi ilizopata kwa ajili ya mabao zaidi.

Alikuwa ni raia wa Ghana Yahya Mohamed aliyetupia bao la pili katika dakika ya 54 kwa kichwa maridadi kilichomshinda Dida ambaye hakuwa na umakini wa kutosha huku akiwa amesogea mbele zaidi ya lango na kushuhudia kichwa kikipigwa mbele yake na kuruka bila mafanikio.

Kinda wa Azam aliyerejea kutoka Mbeya City, Joseph Mahundi anaweza kuwa ndiye aliyefunga bao bora zaidi katika michuano hii, baada ya kupokea pasi akiwa umbali wa zaidi ya mita 25 na kuachia mkwaju mkali wa mbali uliojaa kimiani moja kwa moja na kuiandikia Azam bao la tatu katika dakika ya 80.

Bao la nne limefungwa na kijana toka Medeama ya Ghana Enock Agyei baada ya kumalizia kiufundi pasi ya Afful dakika ya 85, na kufanya ubao usomeke Yanga 0-4 Azam hadi mwisho wa mchezo.

Akizungumzia mechi hiyo Abubakary Salum 'Sure Boy' kwa upande wa Azam amesema siri kubwa ya timu yao kubadilija siku ya leo tofauti na mechi zilizopita ni kuanza kuzoeana kwa wachezaji ambao wengi wao ni wageni.

Naye Saimon Msuva kwa upande wa Yanga amesema wameyapokea matokeo hayo kwa masikitiko makubwa ingawa huo ndiyo mchezo na hayo ni matokeo ya kimcheo na kwamba wanajipanga kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali.

Kwa matokeo hayo Azam wanamaliza wakiwa vinara wa kundi baada ya kukusanya point 7 wakifuatiwa na Yanga wenye point 6 na Zimamoto ina point 3.

Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Zimamoto imeifunga Jamhuri mabao 2-0 huku timu zote zikiaga rasmi mashindano hayo na Jamhuri inaondoka ikiwa na point moja iliyoipata katika mechi yake na Azam, lakini ikiwa haina goli hata moja na Zimamoto imeambulia point 3 ilizopata leo

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu