Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yasubiri barua, M/Kiti aikana kamati saa 72

Alhamisi , 23rd Jan , 2020

Uongozi wa klabu ya Yanga umeendelea kusisitiza kuwa unasubiri barua rasmi ya adhabu iliyotolewa na Kamati ya Uendeshaji wa Ligi kufuatia madai ya utovu wa nidhamu yaliyofanywa na wachezaji wake na kocha.

Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, Stephen Mguto

Akiongea na EATV/Radio Digital, Afisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa wao hawawezi kulalamikia chochote kwa sasa bali wanasubiri barua rasmi kutoka kamati hiyo.

"Siwezi kuzungumzia hilo, sijalalamika na wala Yanga haijalalamika bali  tumesema tunasubiri taarifa tuisome na tujiridhishe na kanuni walizotumia ndio tujue tunakubali au tunakataa", amesema Bumbuli.

Jumatano, Januari 22, Kamati ya Uendeshaji wa Ligi ilitoa adhabu kwa kuwafungia mechi 3 na faini ya Sh. 500,000 wachezaji Kelvin John na Majaliwa Shaban wa Mbeya City na Mrisho Ngassa, Ramadhani Kabwili na Cleafas Sospeter wa Yanga kwa kosa la kugoma kuingia vyumba vya kubadilishia nguo, huku pia ikitoa onyo kwa kocha wa Yanga, Luc Eymael kutokana na kauli yake kwa mwamuzi.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, Stephen Mguto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uendeshaji amesema kuwa kamati hiyo ya maamuzi haiitwi 'kamati ya saa 72' kama inavyoitwa na watu wengi.

"Hii sio Kamati ya saa 72 kama watu wanavyopenda kuiita, hii ni kamati ya uendeshaji wa ligi lakini kuna watu tu na utashi wao walitaka maamuzi yafanyike kwa uharaka zaidi ndio wakaita hivyo", amesema Mguto.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava