Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

KMC kuongeza wachezaji watatu dirisha dogo

Ijumaa , 30th Dec , 2022

Kocha Mkuu wa KMC FC, Thierry Hitimana, amethibitisha kuwa yupo kwenye mpango wa kukiboresha kikosi chake kwa kufanya usajili wa Wachezjai watatu, katika kipindi hiki cha Dirisha dogo la Usajili.

Hitimana amekiri kuwa katika Mchakato huo, kufuatia mapungufu yaliyojitokeza kwenye kikosi chake, kufuatia baadhi ya Wachezaji kuwa Majeruhi wa muda mrefu.

Kocha huyo kutoka nchini Burundi amesema tayari ameshawasilisha ripoti kwa uongozi wa juu, na ana imani watayafanyia kazi, ili wawe imara na kufanya vizuri katika michezo iliyosalia ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Tanzania Bara ‘ASFC’.

“Tumecheza michezo 18 ya Ligi, tumeona madhaifu yetu na wapi tunatakiwa kuongeza nguvu, tayari nimekabidhi Ripoti kwa kutaja nafasi ninazohitaji kusajili kwa lengo la kuisaidia timu kufanya vizuri,”

“Nina imani kubwa na Viongozi wangu watafanikisha hili kwa wakati ili tuweze kuwa na kikosi kitakachoweza kupambana hadi mwishoni mwa msimu huu kwa kufikia malengo tuliojiwekea.” amesema Hitimana.

Hitimana ameongeza bado malengo ya KMC FC ni kumaliza msimu katika nafasi tano za juu, na hilo haliwezi kukamilika kama hawataboresha kikosi chao.

KMC FC inashika nafasi ya tisa katika Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ikiwa imecheza michezo 18 ikiwa na alama 22, ikishinda michezo mitano, Sare saba na imepoteza michezo sita.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto