Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TFF yataka ligi za wilaya kuhusisha zaidi vijana

Ijumaa , 25th Nov , 2022

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limevitaka vyama vya soka nchini vinavyosimamia ligi za Wilaya na Mikoa kuwatumia zaidi wachezaji vijana wenye umri chini ya miaka ishirini (U20) ili kusaidia kuibua , kuvitengeza, kuvikuza na kuviendeleza vipaji vya vijana wengi nchini

Hayo aliyasema Rais wa TFF  Wallace Karia   wakati akitoa hotuba yake mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 17 wa TFF uliofanyika Jijini Mwanza; moja kati ya malengo ya mkutano huo ni pamoja na kufanya tathimini katika utekelezaji wa mipango inaaksi na malengo ya TFF kwa kipindi cha mwaka mzima.

Akieleza kuhusu umuhimu wa ligi hizo kwa daraja la Wilaya na Mikoa Rais Karia alisema kuwa kumekuwa na kasumba ya kuwatumia wachezaji wakubwa na baadhi yao wanaotoka kwenye timu za madaraja ya juu ambao hupatiwa nafasi na kipaumbele kwenye ligi hizo jambo ambalo linarudisha nyuma juhudi za Shirikisho katika kuendelea kuibua vipaji kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, na baadala yake kuendelea kuwatumia wachezaji wale wale ambao tayari wamekwisha tumika kwa muda mrefu.

Alisema kufanya hivyo ni kuwakosesha nafasi wachezaji chipukizi ambao hapo baadaye wanaweza kuwa na msaada mkubwa kwenye timu za Taifa. Hivyo, ameviagiza vyama vya mpira wa miguu nchini  hasa katika ngazi za Wilaya na Mikoa kuhakikisha ligi hizo zinatoa nafasi kwanza kwa wachezaji wa U20 kabla ya kuwatazama wengine.

Aidha, Rais Wallace Karia alieleza sababu za kufanyika kwa Mkutano huo wa kila mwaka mapema zaidi kuwa ni kutokana uwepo wa michuano mikubwa ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 20, 2022 huko Qatar. Alibainisha kuwa TFF imelitizama hilo kwa jicho la tatu kutokana na ukweli kuwa wadau wengi wa soka macho na masikio yao wameyaelekeza kwenye Kombe la Dunia; kwa hiyo, isingekuwa vema kugonganisha ratiba hiyo na jambo kubwa kama hilo la Mkutano Mkuu wa Shirikisho.

Hata hivyo,  Rais Karia aliweka wazi kuwa michezo ya Ligi Kuu ya NBC haitasimama kupisha Kombe la Dunia, baadala itaendelea kama kawaida kutokana na ukweli kwamba hakuna timu ya Ligi Kuu Tanzania yenye wachezaji wengi wanaotakiwa na timu zao za Taifa kama Kanuni za TFF na Bodi ya Ligi zinavyoelekeza. Hivyo, ratiba ya Ligi Kuu itaendelea kama ilivyopangwa na hakutokuwa na mabadiliko yanayotokana na uwepo wa michuano hiyo ya Dunia.

Mkutano Mkuu wa TFF wa namna hii hufanyika kila mwishoni mwa  Mwaka na hii ni kwa mujibu wa Katiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania. Mkutano huu kwa kawaida huhudhuriwa na wajumbe halali na viongozi wenye mwaliko maalum kutoka Taasisi za soka na Serikali pia.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava