Jumatano , 6th Jul , 2022

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson anapambania nafasi yake baada ya viongozi wake wajuu wapatao wawili kujizulu huku wakiukandia uongozi wake.

Kansela Rishi Sunak ambaye ni  waziri wa fedha  pamoja na waziri wa afya nchini humo Sajid Javid wamejiuzulu wakipishana dakika 10 tu wakati wakitangaza maamuzi yao, huku mawaziri wengine wadogo nao wakijuzulu.     

Idadi inayozidi kuongezeka ya wabunge katika chama chake tawala cha Kihafidhina wanasema, wakati umewadia wa Johnson kujiuzulu.

Lakini Bwana Johnson ameonyesha azma yake ya kutaka kusalia madarakani kwa kumteua Nadhim Zahawi ambaye alikuwa waziri wa elimu, kama waziri mpya wa fedha mbali na kujaza nafasi zengine zilizokuwa zimeachwa wazi. 

Baadae leo Johnson  atafika mbele ya bunge kwa ajili ya kuulizwa maswali.