Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ahadi ya CAG kwa Bunge la Tanzania

Jumatano , 1st Aug , 2018

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG, Prof. Mussa Juma Assad amesema kuwa atahakikisha fedha zote zinatumika ipasavyo na hatoruhusu pesa yoyote kutoka hazina bila ruhusa ya Bunge.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG, Prof. Mussa Juma Assad.

Prof. Assad amesema hayo wakati akizungumzia mafanikio ambayo Tanzania imeyapata kutokana na kuwa moja ya nchi zilizofanya ukaguzi wa Umoja wa Mataifa, jukumu ambalo hivi sasa limebebwa na nchi ya Chile.

Prof. Assad amesema wakaguzi zaidi ya 200 waliohusika katika ukaguzi huo, wamejifunza mbinu za kisasa za ukaguzi, ukiwemo kujengewa uwezo kufanya ukaguzi wa mifumo ya malipo ya kielektroniki na kimtandao bila kuisababishia serikali hasara.

Ukaguzi wa hesabu za Umoja wa Mataifa sio tu umeipatia sifa Tanzania, bali umetujengea uwezo wakaguzi kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali, kufanya udhibiti ambapo kuanzisa sasa tutakuwa tukitoa ripoti ya udhibiti wa fedha zote katika mfuko mkuu wa hazina, ambazo zimetumika bila kuidhinishwa na Bunge”, amesema CAG.

Kwa mujibu wa ripoti ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ya mwaka 2016/17 aliyoiwasilisha mwezi Machi, 2018 imeibua ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha katika baadhi ya taasisi za Serikali na kuzua mjadala mkubwa miongoni mwa wananchi.

Ripoti hiyo iliwasilishwa kwa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam ambayo ilizitaja taasisi zilizobainika kuwa na ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha kuwa ni, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali