Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bei ya mafuta yapaa

Jumanne , 7th Aug , 2018

Bei za mafuta ya Petroli, Dizeli na mafuta ya meli visiwani Zanzibar zimeshuka huku bei ya mafuta ya taa ikitajwa kupanda kwa asilimia 4 mwezi Agosti na kufikia kuuzwa shilingi 1,854 kwa lita.

Kituo cha kutolea huduma ya mafuta

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha uhusiano kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji Zanzibar (ZURA), Khuzaimat Bakar na wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari na kusema bei hizo mpya zitaanza kutumika rasmi leo Agosti 07, 2018 katika vituo vyote vya kuuzia mafuta visiwani Zanzibar.

"Bei ya reja reja mafuta ya taa kwa mwezi wa Agosti, 2018 imepanda kwa shilingi 77 kwa lita kutoka shilingi 1,777 kwa lita mwezi Julai, 2018 hadi shilingi 1,854 katika mwezi wa Agosti sawa na asilimia 4. Mafuta ya Petrol kwa bei ya reja reja kwa mwezi Agosti yameshuka kwa shilingi 25 kwa lita kutoka shilingi 2,435 ya mwezi Julai, 2018 hadi shillingi 2,410 kwa lita mwezi Agosti, 2018 ambayo sawa na asilimia 1", amesema Khuzaimat.

Pamoja na hayo, Khuzaimat ameendelea kufafanua kuwa "bei ya reja reja ya dizeli kwa mwezi Agosti imeshuka kwa shilingi 35 kwa lita kutoka shilingi 2,430 ya mwezi Julai hadi shilingi 2395 sawa na asilimia 1.4".

Mbali na bei hizo, pia Khuzaimat amesema bei ya mafuta ya meli yameshuka kwa mwezi Agosti kwa shilingi 36 kwa lita kutoka shilingi 2,259 kwa lita katika mwezi Julai, 2018, hadi shilingi 2,222 katika mwezi Agosti sawa na asilimia
1.5.

Kushuka kwa baadhi ya bei hizo kunatokana mabadiliko ya mauzo ya mafuta hayo katika soko la dunia.

Bei ya Mafuta ya Petroli katika soko la dunia kwa mwezi wa Julai, 2018 imeshuka kwa shilingi 13 sawa na asilimia 1, bei ya mafuta ya Dizeli ikishuka kwa shilingi 33 sawa na asilimia 2.5, bei ya mafuta ya meli kushuka kwa shilingi 33 sawa na asilimia 2.5  huku bei ya mafuta ya taa yakiwa yamepanda kwa shilingi 107 sawa na asilimia 9.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi