Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

FCC na ZFCC zajipanga kudhibiti bichaa bandia 

Alhamisi , 26th Mei , 2022

Tume ya ushindani FCC kwa kushirikiana na Tume ya ushindani halali ya Zanzibar ZFCC zimejipanga kudhibiti uingizaji na uzalishaji wa bidhaa bandia ili kuchochea uchumi utakaolinda soko la ndani na Kumlinda mlaji 

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) William Erio amesema hayo wakati wa kuhutimisha ziara ya kikazi ya siku tatu kwaajili ya kutembelea  Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) ikiwa na lengo la kuimarisha mahusiano na kuangalia namna bora ya kutekeleza majukumu yao.

"Suala la biashara  si suala la muungano, kwahiyo sisi FCC tunashughulika na masuala haya ya kibiashara kwa maana ya kushajihisha ushindani, kulinda washindani katika shughuli zao na kumlinda mlaji kwa Tanzania bara ambapo na wenzentu wanafanya hivyohivyo kwa upande wa Tanzania Zanzibar" Alisema William Erio ambaye ni Mkrugenzi Mkuu Tume ya ushindani Tanzania FCC

Aidha Mkurugenzi huyo alisema Serikali ya awamu ya sita imejikita katika kuimarisha uwekezaji Kama njia mojawapo Kuu ya kuleta mitaji na kukuza uchumi wa nchi yetu Kama vile inavyofanya serikali ya awamu ya nane kule Tanzania Zanzibar.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani halali ya biashara Mohammed Sijari Mohammed amesema  kuwa Zanzibar inaendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kufanya mapitio ya baadhi ya sheria ikiwemo sheria ya maendeleo ya viwanda ambayo itawezesha wananchi kunufaika  na bidhaa zinazozalishwa viwandani.

"Kwa upande wa Zanzibar kuna jitihada kubwa zinafanyika za makusudi kwake Mhe. Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi kwa kuweka mazingira bora ya biashara na kudhibiti ushindani" alisema Mohammed Sijari Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani - ZFCC

Miongoni mwa mambo ambayo ZFCC imejifunza kutoka Tume ya Ushindani Bara ni pamoja na masuala ya ukaguzi na udhibiti wa bidhaa bandia ,taratibu za kanuni na sheria ,na masuala ya muunganiko baina ya kampuni.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton