Jumanne , 29th Nov , 2022

Wafanyabiashara wa maeneo mbalimbali nchini wameiangukia serikali, wakiomba kufikiwa na mikopo ya Halmashauri ili waachane na mikopo umiza ambayo imekuwa ikiua biashara zao.

Mwanne Mohamed, mama n’tilie

EATV imefika imetembelea maeneo mbalimbali jijini Dar, na kuzungumza na wafanyabiashara wadogo, zaidi wanaeleza mikopo hiyo ambayo imekuwa ikiharibu maisha yao.

EATV imemtafuta Mtaalam wa masuala ya Uchumi, kulifafanua su-ala hili, ambapo amebainisha kuwa changamoto hii inatokana na kukosekana kwa elimu ya fedha kwa wananchi wenye uhitaji wa mikopo hiyo.

Aidha Nguma ameshauri Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusimamia taratibu za utolewaji mikopo hiyo, ili iwafikie walengwa.