Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Tanga wana mzigo uliopita" - EWURA

Jumatatu , 10th Sep , 2018

Imeelezwa kuwa tofauti ya bei za mafuta kati ya Dar es salaam na Tanga ni kutokana na mkoa huo kuwa na mafuta ambayo yalinunuliwa kwa bei kubwa mwezi Mei ambayo mpaka sasa shehena yake haijaisha na si kwamba bei zimepanda kama inavyodaiwa.

Pichani gari likijazwa mafuta.

Akizungumza kwenye East Africa BreakFast ya East Africa Radio, afisa habari wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Titus Kaguwo amesema kuwa bandari inayolisha mikoa ya Kaskazini bado haijamaliza mafuta yaliyochukuliwa kwa gharama kubwa na itapungua wakimaliza na kuagiza mapya.

Sasa hivi tunatumia bandari tatu, zikiwemo bandari ya Dar es salaam, Mtwara na Tanga na matumizi ya kila bandari yanatofautiana kutokana na idadi ya watu na matumizi yake, Dar es salaam inahudumia sehemu kubwa ya nchi hivyo mzigo ulioingia kwa gharama kubwa umeshakwisha lakini Tanga bado wana mzigo uliopita wala bei haijapanda”, amesema Kaguwo.

Septemba 5, 2018 Ewura ilitangaza kushuka kwa bei za rejareja za Petroli, Dizeli na mafuta ya Taa kwa asilimia 0.43 (shilingi 10) na asilimia 0.83 (shilingi 19) na asilimia 1.05 (shilingi 24 kwa lita) huku bei za rejareja za Petroli na Dizeli kwa Mikoa ya Kaskazini zimeongezeka kwa shilingi 114/lita (sawa na asilimia 5.11) na shilingi 102/lita (sawa na asilimia 4.70).

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa