Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TBL yashinda tuzo ya kimataifa

Jumatano , 26th Feb , 2020

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imepata Tuzo ya kimataifa ya Kizibo Cha Dhahabu (IGCA) inayomaanisha Ubora wa Kimataifa kutokana na uzalishaji wa bidhaa zake bora.

Mfano wa tuzo hiyo.

TBL YASHINDA TUZO YA KIMATAIFA YA KIZIBO CHA DHAHABU, KUKIONESHA KWA WATANZANIA

Februari 26, 2020: Dar es Salaam: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imepata Tuzo ya kimataifa ya Kizibo Cha Dhahabu (IGCA) inayomaanisha Ubora wa Kimataifa kutokana na uzalishaji wa bidhaa zake bora. Hii ndio mara ya kwanza kwa bara la Afrika kupata tuzo hii. Inakadiriwa kuwa kilo 16.01 za dhahabu ambayo kwa bei za kimataifa ni sawa na Bilioni 2 za kitanzania.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Brand za TBL, Pamela Kikuli alisema kuwa, TBL imefurahi kupata tuzo hiyo ambayo alisema kuwa imeongeza heshima katika jina la kampuni na bidhaa zake na kwamba wataendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kukidhi mahitaji ya wateja wake nchini kote.

“Kwakweli tumefurahi sana kupata tuzo hii ambayo ni ya kimataifa. Kila mara tunafikiria kuendelea kuwa vinara katika soko. Ndiyo maana bidhaa zetu zinakuwa na ladha na ubora wa kimataifa vitu ambavyo vinawavutia wateja wetu katika soko la Tanzania.” Aliongeza.

Bi. Pamela alisema pia kuwa, kwa kuwathamini wateja wake tuzo hiyo itapelekwa katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ili kuwapa fursa ya kushuhudia tuzo hiyo.

Kwa mujibu wa Kikuli, tuzo hiyo siku ya alhamisi tarehe 27 kizibo chetu cha dhahabu kitaoneshwa makutano ya barabara ya Karume, Ilala kuanzia saa 1:00 kamili asubuhi hadi 8:00 mchana ambapo wateja mbalimbali na wananchi kwa ujumla watapata fursa ya kuiona na hata wengine kupiga nayo picha kisha kuelekea eneo la Biafra, Kinondoni na kuoneshwa kuanzia saa 9:00 mchana hadi saa 1:00 kamili jioni.  Ziara ya maonesho ya kizibo itaishia siku ya Ijumaa, tarehe 29 katika eneo la makutano ya barabara eneo la makutano ya barabara Buguruni kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 1:00 jioni. Lengo letu ni kusherehekea na wateja wetu ambao ndiyo wametufikisha hapa tulipo,” alisema Kikuli.

Bidhaa zinazozalishwa na TBL ni pamoja na Safari Lager, Kilimanjaro Premium Lager, Ndovu Special Malt, Castle LITE, Castle Lager, Castle Milk Stout, Redds Original, Budweiser, Balimi Extra Lager, Eagle Lager, Grand Malt na Safari Sparkling Water.

TBL group imeorodheshwa katika soko la hisa la Dar es Salaam, ikiwa na wafanyakazi takriban 1,700, inafanya uzalishaji katika mikoa minne ikiwa na vituo kadhaa vya usambazaji wa bidhaa zake.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri